Jumamosi, 19 Oktoba 2019

MAMA MWANAMWEMA SHEIN-AFUNGUA KONGAMANO LA WAJASIRIAMALI WA UWT UNGUJA.


 MKE  wa Rais wa Zanzibar, Mama Mwanamwema Shein akisalimiana na Makamu Mwenyekiti wa UWT Taifa Thuwayba Kisasi mara baada ya kuwasili katika ufunguzi wa  Kongamano la Mafunzo ya Ujasiriamali kwa Wanawake wa Mikoa ya Unguja yaliyoandaliwa na UWT  Zanzibar  na kufanyika katika Ukumbi wa Dk.Ali Mohamed Shein SUZA-Tunguu.

  MKE  wa Rais wa Zanzibar, Mama Mwanamwema Shein akisalimiana na Viongozi mbali mbali wa UWT na Serikali walioudhuria katika Ufunguzi huo wa Mafunzo ya Ujasiriamali.

  MKE  wa Rais wa Zanzibar, Mama Mwanamwema Shein akikagua bidhaa mbali mbali zilizotengenezwa na Wajasiriamali hao wa Mikoa ya Unguja.






  MKE  wa Rais wa Zanzibar, Mama Mwanamwema Shein akielezwa Huduma zinazotolewa na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF), ambao ni moja ya Shirika lililodhamini Mafunzo hayo ya Ujasiriamali.

 BAADHI ya Wadhamini wa Mafunzo ya ujasiriamali yaliyoandaliwa na UWT Zanzibar ambao ni Taasisi ya Viwango Zanzibar (ZBS) na Shirika la Biashara Zanzibar (ZSTC) wakiwa katika maonyesho hayo.

 BAADHI ya Viongozi na Wanachama wa CCM na Jumuiya zake wakisikiliza nasaha za Viongozi mbali mbali zinazotolewa katika Ufunguzi wa Mafunzo ya Ujasiriamali kwa Wajasiriamali wa Zanzibar.


Makamu Mwenyekiti wa UWT Taifa.Bi.Thuwaiba Edington Kisasi,akizungumza katika kongamano hilo na kuwasisitizi Vijana na Akina Mama Mijini na Vijijini kuchangamkia fursa mbali mbali zinazopatikana katika Ujasiriamali ili wajikwamue kiuchumi na kujiongezea kipato.

 NAIBU Katibu Mkuu wa UWT Zanzibar Ndugu Tunu Juma Kondo, akizungumza na kuwakaribisha Viongozi na Waalikwa mbali mbali katika Ufunguzi wa Kongamano hilo la Ujasiriamali lililofanyika  katika Ukumbi wa Dk.Ali Mohamed Shein SUZA-Tunguu.

 Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein akihutubia wakati akilifungua Kongamano la Wajasiriamali Wanawake Zanzibar linalofanyika katika ukumbi wa mkutano wa Dk. Ali Mohamed Shein Tunguu (SUZA) kulia Waziri wa Kazi Uwezeshaji Wazee Wanawake na Watoto Zanzibar.Mhe. Maudline Castico na kushoto Makamu Mwenyekiti wa UWT Taifa.Bi.Thuwaiba Edington Kisasi, ufunguzi huo umefanyika leo.19-10-2019.  


MKE  wa Rais wa Zanzibar, mama Mwanamwema Shein amesema shughuli za ujasiriamali zinahitaji taaluma ili ziweze kufanyika kwa ufanisi na kuleta tija pamoja na kuondokana na changamoto.

Mama Mwanamwema amesema hayo katika ufunguzi wa Kongamano la  Wajasiriamali wanawake wa Mikoa ya Unguja, hafla iliyofanyika katika Ukumbi wa Dk. Ali Mohamed Shein, SUZA - Tunguu, Mkoa wa Kusini Unguja.

Amesema shughuli za ujasiriamali kama ilivyo shughuli nyengine zinahitaji elimu ya nadharia na vitendo ili kumwezesha mjasiriamali kupata tija na kuongeza kipato katika familia.

Amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Awamu ya saba inayoongozwa na Rais Dk. Shein imeunda Wizara ya Kazi, Uwezeshaji, Wazee, wanawake na watoto, pamoja na kaunzisha Mfuko wa Uwezeshaji wa wananchi kiuchumi ili kufanikisha azma ya kukuza Sekta ya ujasiriamali.

Ameeleza kuwa Serikali imeandaa mipango mbali mbali ya kuwasaidia wananchi ili kuongeza kipato, hivyo akawataka wananchi kuzitumia ipasavyo fursa zilizopo ili kuongeza kipato cha familia.
Aidha, Mama Mwanamwema ameipongeza Jumuiya ya Wanawake Tanzania (UWT), kw uamuzi wa kuandaa kongamano hilo, ambapo pamoja na mambo mengine linazungumzia umuhimu wa kuimarisha Daftari la wapiga kura.

Alisema wakati huu wananchama wa CCM wakiajiandaa kushiriki katika uchaguzi mkuu ujao mwakani, kuna umuhimu wa kukumbushana uimarishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura, hivyo akatowa wito kwa kila mmoja kushiriki na kutekeleza wajibu wake wakati utakapofika.

Amesema ushindi wa CCM utapatikana kupitia uimarishaji wa daftari hilo, kwa msingi kuwa bila ya kujiandikisha hakutakuwa na fursa ya mtu kupiga kura.

Amesema vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia pamoja na matumizi ya dawa za kulevya  ni mambo yanayohitaji mikakati mizuri ya  haraka katika kupambana navyo.

Mama Mwanamwema amewataka washirki wa kongamano hilo kuwa makini na watulivu katika kipindi chote cha mafunzo ili kufikia malengo yaliokusudiwa, sambamba an kuwapongeza wafadhali mbali mbali waliowezesha kufanyika kongamano hilo.

Nae, Waziri wa Kazi, Uwezeshaji, Wazee, wanawake na watoto Moudline Castico, alimpongeza Mama Mwanamwema kwa mchango mkubwa anautowa katika kusaidia harakati za ujasiriamali kwa akinamama.

Akizungumza Makamu Mwenyekiti wa UWT Taifa, Thuwayba Edington Kisasi, amesema lengo la Jumuiya hiyo kuhakikisha wananchi wote wanapata elimu ya ujasiriamali nchi nzima.

Amewata washiriki wa mkongamano hilo kuitafutia ufumbuzi changamoto ya udhalilishaji wa kijinsia, akibainisha chanzo chake kinatokana na jamii kuondokana na utamaduni, mila na silka za Wazanzibari.

Ndugu Thuwayba amewapongeza wafadhali mbali mbali, ikiwemo ZRB, NMB, ZSSF, ZURA, Bima, Chuo Kiku cha Taifa SUZA na wengineo kwa michango yao iliyofanikisha kufanyika kongamano hilo.

Mapema, katika hafla hiyo Mama Mwanamwema amekagua bidhaa mbali mbali zinazozalishwa na vikundi vya ujasiriamali kutoka Mikoa hiyo ya Unguja.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni