Jumapili, 27 Oktoba 2019

NDG.CASSIAN -AZINDUA KITUO CHA UJASIRIAMALI JANG'OMBE.


 KATIBU wa Kamati Maalumu ya NEC,idara ya Organazesheni CCM Zanzibar ndugu Cassian Galos Nyimbo(wa pili kutoka kulia),akikata utepe kuashiria ufunguzi wa Kituo cha mafunzo ya ujasiriamali cha Jimbo la Jang'ombe,Mwakilishi wa Jimbo hilo Mhe.Ramadhan Hamza Chande (wa kwanza kushoto) na Katibu wa Siasa na Uenezi wa CCM Jimbo hilo (wa kwanza kutoka kulia).
KATIBU wa Kamati Maalumu ya NEC,idara ya Organazesheni CCM Zanzibar ndugu Cassian Galos Nyimbo akihutubia wananchi katika uzinduzi wa Kituo cha ujasiriamali Jang'ombe.
MWAKILISHI wa Jimbo la Jang'ombe Mhe.Ramadhani Hamza Chande,akizungumza katika hafla hiyo.




BAADHI ya Waalikwa na wanafunzi wa kituo hicho wakisikiliza nasahas mbali mbali kutoka kwa viongozi wa JImbo la Jang'ombe.

MWENYEKITI wa UVCCM Mkoa wa Mjini ndugu Kamaria Suleiman Nassor,akitoa shukrani katika hafla hiyo.

KATIBU wa Siasa na Uenezi CCM Jimbo la Jang'ombe akizungumza katika hafla hiyo.


KATIBU wa Kamati Maalumu ya NEC,idara ya Organazesheni CCM Zanzibar ndugu Cassian Galos Nyimbo,amewataka Wanawake na Vijana wa jimbo la jang'ombe kutumia vizuri fursa ya ujasiriamali kwa kujiajiri wenyewe.

Wito huo ameutoa wakati akizindua Kituo cha Mafunzo ya Ujasiriamali cha Jimbo la Jang'ombe kilichoanzishwa na Mwakilishi wa Jimbo hilo uko Kilimani Mnara wa mbao Unguja.

Amesema ujasiriamali ni kazi kama zilivyo kazi zingine katika jamii hivyo ujuzi unaotokana na sekta hiyo unatakiwa kuthaminiwa na kupewa kipaumbele.

Galos ameeleza kuwa mafunzo hayo ya ujasiriamali watakayopewa wananchi wa jimbo hilo kupitia Kituo hicho yawe na tija ya kujikwamua kichumi na kujiongezea kipato.

Katika maelezo ya Katibu huyo, amempongeza Mwakilishi huyo kwa ubunifu wake wa kuanzisha Kituo kitakachozalisha wataalumu wengi wa masuala ya ujasiriamali wenye uwezo wa kutengeneza bidhaa mbali mbali zenye viwango.

Naye Mwakilishi wa Jimbo la Jang'ombe Mhe.Ramadhani Hamza Chande,alisema lengo la kuanzisha kituo hicho ni kuwapatia ujuzi wa masuala ya ujasiriamali wananchi wa jimbo hilo hasa vijana na wanawake.

Amesema wakati alipokuwa akiomba wananchi wampatie ridhaa ya uongozi aliahidi kuanzisha kituo hicho cha kutoa mafunzo ya ujasiriamali na kwa sasa tayari ametekeleza ahadi hiyo.

Amesema katika Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2015/2020 imeelekeza uanzishwaji wa vituo vya mafunzo  ya ujasiriamali nchini, hivyo jimbo hilo wametekeleza maelekezo ya Ilani.

Amesema kituo kimesajiliwa na kupitia taratibu zote za kisheria pia wana wakufunzi waliobobe katika kufundisha utengenezaji wa bidhaa bora zinakubalika katika soko la ndani na kimataifa.

Aidha ameeleza kuwa kituo hicho kwa awamu ya kwanza kinatarajia kutoa Wanafunzi zaidi ya 300 na kitakuwa ni endelevu.

Akitoa shukrani katika hafla hiyo Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Mjini ndugu Kamaria Suleiman Nassor, amewapongeza viongozi wa jimbo la Jang'ombe kwa ushirikiano wao uliozaa matunda ya kuanzisha kituo hicho kitakachowanufaisha Vijana wengi.

Amewasihi vijana wa jimbo hilo kuchangamkia fursa hiyo kwa kujiunga kituo hicho ili wapate ujuzi utakaowawezesha kutengeneza bidhaa zitakazowapatia kipato.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni