Jumamosi, 26 Oktoba 2019

MHE.RAMADHAN HAMZA CHANDE -AZING'ARISHA MASKANI ZA CCM JANG'OMBE.



MWAKILISHI wa Jimbo la Jang'ombe Mhe.Ramadhani Hamza Chande (kushoto) ,akimkabidhi mabati saba ya kuezekea maskani ya Bora Imani iliyopo Urusi Jang'ombe ndugu Omar Said Salum 'Saa nane' (wa nne kutoka kulia)

MWAKILISHI wa Jimbo la Jang'ombe Mhe.Ramadhani Hamza Chande (kushoto) , akimkabidhi fedha taslimu shilingi 70,000 Mjumbe wa maskani ya Karume ndugu Ibarahimu Abass Faki kwa ajili ya matengenezo ya maskani hiyo.
 MWAKILISHI wa Jimbo la Jang'ombe Zanzibar Mhe.Ramadhan Hamza Chande (kushoto), akimkabidhi fedha na mabati Katibu wa Masskani ya Buda iliyopo Ziwani Ndugu Ramadhan Salmin Songoro.

 KATIBU wa Siasa na Uenezi CCM Jimbo la Jang'ombe ndugu Ali Ahmad Ibrahim akizungumza na Wana Maskani ya Ramadhan Hamza Chande katika ziara ya Mwakilishi huyo ya kutembelea maskani za CCM. 



 MWAKILISHI wa Jimbo la Jang'ombe Zanzibar Mhe.Ramadhan Hamza Chande akiwa na viongozi na wanachama wa maskani Buda.

 MWAKILISHI wa Jimbo la Jang'ombe Zanzibar Mhe.Ramadhan Hamza Chande akikabidhi Mabati kwa Uongozi wa Maskani ya Mtundani iliyopo Matarumbeta Jang'ombe Zanzibar.

 MWAKILISHI wa Jimbo la Jang'ombe Zanzibar Mhe.Ramadhan Hamza Chande akizungumza na Wana maskani ya  CCM Kidongochekundu Zanzibar.


MWAKILISHI wa Jimbo la Jang'ombe Zanzibar Mhe.Ramadhan Hamza Chande (kushoto),akimkabidhi seti moja ya jezi Meneja wa timu ya mpira wa miguu ya Kidongo chekundu City ndugu Omar Shamna (kulia).
 KATIBU wa Siasa na Uenezi CCM Jimbo la Jang'ombe ndugu Ali Ahmad Ibrahim akizungumza n Wana Maskani ya CCM ya Ramadhan Chande katika ziara ya Mwakilishi huyo katika Jimbo hilo.
MWAKILISHI wa Jimbo la Jang'ombe Mhe.Ramadhani Hamza Chande  akikabidhi Uongozi wa Maskani ya Ramadhan Hamza Chande Mabati ya kuezekea Maskani hiyo.

MWAKILISHI wa Jimbo la Jang'ombe Zanzibar Mhe.Ramadhan Hamza Chande, ametoa vifaa vyenye thamani ya zaidi ya Shilingi milioni 1.5 kwa maskani nane za Chama Cha Mapinduzi zilizomo katika jimbo hilo.

Akizungumza katika mwendelezo wa ziara zake katika maskani mbali mbali za CCM jimboni humo, Mhe.Ramadhani amesema vifaa hivyo ambavyo ni Mabati ya kuezekea nyumba, Jezi za mpira wa miguu na fedha taslimu ni sehemu ya utekelezaji wa ahadi zake alizowaahidi wananchi katika kampeni za uchaguzi zilizopita.

Alisema kwamba wakati akiomba ridhaa ya wananchi katika jimbo hilo aliahidi kuzipatia vifaa hivyo maskani za Chama Cha Mapinduzi zilizokuwa na changamoto mbali mbali  zilizotakiwa kutatuliwa na viongozi wa Chama.

Alieleza kuwa katika uongozi wake ndani ya jimbo hilo ataendelea kuwa karibu na Wananchi wa makundi yote, bila kubagua rika zao kwani kila mmoja ana umuhimu wake katika maisha ya kisiasa.

Katika maelezo yake Mwakilishi huyo Mhe.Ramadhan, aliwambia viongozi na makada wa maskani hizo kuwa Chama Cha Mapinduzi kinawathamini kutokana na mchango wao wa kuimarisha taasisi hiyo Kisiasa na Kiuchumi.

Alitoa nasaha zake kwa  wanachama mbali mbali wa maskani hizo kubuni miradi  ya ujasiriamali ili Vijana,Wanawake na Wazee wapate sehemu mbadala ya kujiingizia kipato.

Katika ziara hiyo aliwakumbusha Wananchi hasa Wana CCM kuhakiki vitambulisho vyao vya mzanzibar mkaazi sambamba na kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura ili wapate uhalali kukipigia kura Chama Cha Mapinduzi na kuhakikisha kinashinda katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2020.

Alieleza kwamba kutokana na kazi aliyopewa na Wananchi wa Jimbo hilo ametekeleza Ilani ya Chama kwa zaidi ya asilimia 70 na anaendelea kukamilisha ahadi zake ili ifika mwishoni mwa mwezi Desemba awe amemaliza utekelezaji wa ahadi zake.

"Nawashukru sana Viongozi wenzangu wa jimbo letu wakiwemo mbunge ,madiwani na viongozi wote wa Chama na Jumuiya zake kwa ushirikiano wenu, ulioteta tija kubwa kwa wananchi wetu wote.

Naye Diwani wa wadi ya Kwaalinatu Mhe.Fatma Suleiman Juma, amewataka wananchi kuendelea kujali na kuitunza  miradi ya maendeleo inayotekelezwa na viongozi wa CCM ili idumu kwa muda mrefu kwa maslahi ya vizazi vijavyo.

Kwa upande wake Diwani wa wadi ya Urusi Mhe.Ibrahimu Abass Faki, amesema kwamba jimbo hilo limeendelea kuimarika kimaendeleo kutokana na ushirikiano wa viongozi wake katika kutekeleza Ilani ya CCM.

Akizungumza Katibu wa Siasa na Uenezi wa Jimbo hilo Ali Ahmad Ibrahim, amesema ziara hiyo imeongeza hamasa kubwa wa wana maskani hao kwani changamoto zao za muda mrefu zimetafutiwa ufumbuzi na kudumu na mwakilishi huyo.

Ameongeza kuwa kila mwanachama na viongozi wa CCM ndani ya jimbo hilo anatakiwa kuandaa vizuri zana zake za mapambano ya vita ya kisiasa kuelekea 2020,kwani muda kusema kwa maneno umepita na kilichobaki ni kutekeleza kwa vitendo.

Naye Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Mjini kichama ndugu Habiba Nasib Suleiman, amemshukru Mwakilishi huyo kwa kutekeleza Ilani ya CCM na kuwataka Viongozi wengine wa Wilaya hiyo kufuata nyayo za kiongozi huyo kwa kuwafuata wananchi katika maeneo yao ili kutatua changamoto zinazowakabili.


























Hakuna maoni:

Chapisha Maoni