Jumanne, 8 Mei 2018

DK.SHEIN AZUNGUMZA NA MABALOZI WILAYA YA DIMANI, ASEMA MAFANIKIO NI MENGI KULIKO CHANGAMOTO

 MAKAMU Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akiwahutubia mabalozi wa CCM Wilaya ya Dimani.

 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Mabodi akizungumza kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar  Dk.Ali Mohamed Shein katika ziara yake ya kuzungumza na mabalozi wa CCM Wilaya ya Dimani.

 MWENYEKITI wa CCM Mkoa wa Magharibi Mohamed Rajab Sudi akizungumza na mabalozi wa CCM Wilaya ya Dimani.

 MABALOZI wa CCM wilaya ya Dimani wakifuatilia kwa kina hotuba ya Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein.

BAADHI ya viongozi na mabalozi wa CCM Wilaya ya Dimani wakiimba wimbo wa mashujaa wa Zanzibar katika ziara ya Dk.Shein ya kuzungumza na mabalozi wa Wilaya ya Dimani.

 MWENYEKITI wa CCM Wilaya ya Dimani Hussein Ali Mgema 'Kimti' akizungumza na mabalozi wa wilaya hiyo katika ziara ya Dk.Shein.

 MSOMA risala ya mabalozi wa Wilaya ya Dimani Mwanakheir Iddi akisoma risala hiyo kwa mgeni rasmi Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein.





MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dk.Ali Mohamed Shein amesema serikali ya awamu ya saba chini uongozi wake ametekeleza Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015/2020 kwa kiwango kikubwa kwa lengo la kumaliza changamoto zinazowakabili wananchi.

Pia amesema  mafanikio yaliyotokana na utekelezaji huo wa sera imara za Chama Cha Mapinduzi ni makubwa kuliko changamoto zilizobaki kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2020.

Hayo ameyasema wakati akizungumza na mabalozi wa CCM Wilaya Dimani katika ukumbi wa CCM Mkoa wa Mjini uliopo Amani Unguja, alisema serikali imeimarisha sekta za afya, elimu, maji safi na salama,umeme  pamoja na ukarabati na ujenzi wa barabara za kisasa.

Amesema serikali inaendelea na mikakati ya kumaliza tatizo la kujaa maji katika eneo la Mwanakwerekwe sokoni kwa kuanza ujenzi wa kuinua barabara kutokea makutano ya barabara  ya Mwanakwerekwe hadi makaburini sambamba na ujenzi wa  mitaro mikubwa itakayopitisha maji kuelekea baarini kupitia shehia za Magogoni, Amani mboriborini hadi Pwani ya kinazini.

Amefafanua kuwa katika kuhakikisha mradi huo unakamilika kabla ya mvua za masika mwaka 2019 kiasi cha Dola za kimarekani milioni 33 zimetengwa ambazo ni mkopo kutoka Benki kuu ya Dunia.

Dk. Shein amesema Serikali pia imedhamiria kutenga bajeti itakayomaliza tatizo la kujaa maji katika maeneo ya kibondemzungu ili kuwaondoshea wananchi usumbufu wanaopata katika mvua za masika.

Katika ziara hiyo aliwataka Mabalozi hao washirikiane na wanachama katika kusimamia utekelezaji wa ilani ya Chama na kuwa karibu na wananchi wa makundi yote.

Nae Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Mabodi amesema Chama Cha Mapinduzi wilaya ya Dimani imepiga hatua katika kuimarisha Chama cha mapinduzi ikiwemo kuvunjwa kwa makundi ya kuharisha uhai wa Chama ndani Wilaya hiyo.

Mapema Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Magharibi Mohamed  Rajab Sudi, ameeleza hali ya kisiasa katika mkoa wake imeimarika kutokana na umoja na mashirikiano yaliyopo kati ya Viongozi wa wanachama na serikali.

Akisoma Risala ya Mabalozi, Mwanakheir Iddi waliipongeza  Serikali kwa kutekeleza miradi ya kimaendeleo jambo ambalo limejenga imani kwa wananchi wa visiwa vya Zanzibar.

Ziara hiyo ya Makamo mwenyekiti CCM Zanzibar  iliyoanza May 2, mwaka 2018 Kisiwani Pemba iliyokuwa na lengo la kuimarisha Chama na kuzungumza na Mabalozi wa Mikoa yote ya Unguja na Pemba imefika tamati May 8, mwaka huu katika Mkoa wa Magharibi kwa kuzungumza na Mabalozi wa Wilaya za  Mfenesini.




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni