Ijumaa, 27 Januari 2017

MKUTANO NA WANDISHI WA HABARI




UTANGULIZI:

ASSALAM ALEYKUM, 

Ndugu Wandishi wa Vyombo mbali mbali vya Habari.
Awali ya yote, napenda nichukue nafasi hii kumshukuru Mwenyezi Mungu, Muumba wa Mbingu, ardhi na vyote viliomo ndani yake, kwa kutujaalia uzima na afya njema. Aidha, nachukua nafasi hii kwa mara nyengine tena kuwashukuru nyinyi waandishi wa vyombo mbali mbali kwa kukubali wito wetu na kuhudhuria kikao hiki.

Ndugu wandishi wa Habari.
Mnafahamu fika kwamba kila ifikapo mwishoni mwa mwezi Januari ya kila mwaka, Chama Cha Mapinduzi huwa kimo katika vuguvgu la kuadhimisha kuzaliwa kwake tangu vyama vya TANU na ASP vilipoungana na kuunda Chama kimoja (CCM) tarehe 5, Februari 1977 tukio ambalo lilifanyika katika Uwanja wa Amani Mjini Zanzibar.



Ndugu wandishi wa Habari.
Sasa Maadhimisho hayo yatafanyika katika ngazi za Mikoa, na tayari kila Mkoa umeshaandaa ratiba za shughuli mbali mbali ambazo watazifanya katika Mikoa yao.
Shughuli hizo ni kama zifuatazo:-
Kutakuwa na zoezi la Usafi wa Mazingira katika maeneo ya Mikoani, Wilayani, Majimboni, Matawini na Maskani za CCM.
1.  Shughuli za kukagua Wagonjwa na kuwafariji Wazee wasiojiweza.
2. Kutakuwa na Mikutano Mikuu ya Ngazi mbali mbali.
3.  Mikutano ya Kamati za Siasa.
4.  Mikutano ya Halmashauri  Kuu za Jimbo.
5.  Zoezi la kupanda miti  katika maeneo mbali mbali ya kijamii  na vyanzo vya Maji.
6.  Kutakuwa na michezo ya aina mbali mbali kama vile  mashindano ya resi za baiskeli, michezo ya nage, michezo ya Bao, Mpira wa Basketboli pamoja na    Mpira wa Miguu.
7.  Makongamano yatakayoelezea historia ya CCM, mafanikio ya miaka 40 ya CCM pamoja na Utekelezaji wa  Ilani ya Uchaguzi ya CCM mwaka 2015 – 2020.

Ndugu Wandishi wa Habari.
Pamoja na mambo yote hayo tuliyoeleza lakini pia yanaweza kujitokeza mengine ambayo hayakutajwa katika taarifa hii, lakini Mikoa watayafanya katika kuadhimisha kuzaliwa kwa CCM kwani mwaka wote huu wa 2017 ni mwaka wa kuadhimisha miaka 40 ya kuzaliwa kwa Chama hicho.

Ndugu Wandishi wa Habari.
Mwisho naomba kutoa wito kwa Wana CCM wote kushiriki kwa wingi katika Mikoa yao kuadhimisha siku hiyo muhimu ya kuzaliwa kwa Chama chetu cha CCM. Aidha, Chama Cha Mapinduzi kinawashukuru kwa dhati kabisa Wana CCM na Wananchi wote wa Jimbo la Dimani pamoja na Kata za  Mikoa ya Tanzania Bara iliofanya Uchaguzi  kwa kupiga kura kwa amani na utulivu mkubwa hatimae kukichagua kwa kishindo kikubwa  Chama Cha CCM, kwa kujua kwamba CCM ndio kimbilio la wanyonge na ni Chama kinachotekeleza Ilani yake ya Uchaguzi kwa makini na kwa wakati.

Baada ya maelezo hayo, nikushukuruni tena kwa kunisikiliza na nikutakieni kila la kheri katika majukumu ya kazi zenu.
Ahsanteni sana.

“KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI”

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni