Jumapili, 23 Septemba 2018

KAMATI MAALUM YA NEC CCM TAIFA Z'BAR YATOA MILIONI TANO KWA AJILI YA RAMBIRAMBI ZA AJALI YA MV.NYERERE.

MAKAMU Mwenyekiti wa CCM Zanzibar ambaye pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein akiongoza Kikao cha Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Zanzibar,  kilichofanyika leo Afisi Kuu ya CCM iliyopo Kisiwandui Zanzibar.
 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk. Abdulla Juma Mabodi akisoma ajenda za Kikao cha Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Zanzibar, kilichofanyika leo Afisi Kuu ya CCM iliyopo Kisiwandui Zanzibar.


 MAKAMU Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein(aliyekuwepo katikati),Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan (wa pili kushoto), Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa ambaye pia ni Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idd(wa kwanza kushoto)pamoja na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla Mabodi(wa kwanza kulia) wakiwa wamesisima kwa ajili ya kutoa heshima na kuomboleza Maafa ya Ajali ya Kivuko cha MV.Nyerere iliyotokea Mkoani Mwanza Septemba 20, mwaka 2018 katika Kikao cha Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Zanzibar kilichofanyika leo katika Afisi Kuu ya CCM iliyopo Kisiwandui Zanzibar.

 MAKAMU Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein akizungumza na Wajumbe wa Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Zanzibar katika Kikao kilichofanyika leo Kisiwandui kwa ajili ya kujadili majina ya Wagombea Uwakilishi wa CCM katika Jimbo la Jang'ombe.

 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk. Abdulla Juma Saadalla (kushoto) akisalimiana na Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idd (kulia) mara baada ya kuwasili Afisi Kuu CCM kwa ajili ya Kikao cha Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Zanzibar.

 MJUMBE wa Kamati Kuu ya CCM Taifa ambaye pia ni Katibu wa Kamati Maalum ya NEC, Idara ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa  CCM Zanzibar Mwl.Kombo  Hassan Juma (kushoto) akisalimiana na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa ambaye pia ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan baada ya kuwasili katika Mkutano wa Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya  CCM  Taifa  Zanzibar. 
 MJUMBE wa Kamati Kuu ya CCM Taifa ambaye pia ni Katibu wa Kamati  Maalum ya NEC, Idara ya Uchumi na Fedha CCM Zanzibar  Ndugu Hafadhali Taibu Hafadhali (kushoto) akisalimiana na Makamu wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idd(kulia) baada ya kuwasili Kisiwandui kwa ajili ya Kikao cha Kamati Maalum ya  Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Zanzibar. 


 MJUMBE wa Kamati Kuu ya CCM Taifa ambaye pia ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akikabidhi Mabati 180 ya kuezekea Tawi la CCM Urusi lililopo Jang'ombe ikiwa ni Utekelezaji wa ahadi zake alizotoa katika ziara yake ya Kichama Zanzibar April 6, mwaka 2018.

Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar akizungumza na Waandishi wa Habari mara baada ya kumaliza kikao cha Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Zanzibar kilichofanyika Kisiwandui. Picha na Afisi Kuu CCM Zanzibar.



KAMATI Maalum ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi(CCM) Taifa Zanzibar,imetoa salamu za rambi rambi kwa Mwenyekiti wa CCM Taifa, Dk.John Magufuli kwa kutokea na ajali ya kivuko cha MV Nyerere ambayo imesababisha vifo vya zaidi ya watu 100 katika kisiwa cha Ukara.

Akitoa salamu hizo leo katika kikao cha Kamati hiyo Mjini Unguja Makamu Mwenyekiti wa CCM, Dk.Ali Mohamed Shein ambaye ni Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
amesema kamati hiyo imesikitishwa na ajali hiyo ambayo imetokea Septemba 20 mwaka huu katika kisiwa hicho Mkoani Mwanza.

Makamu huyo Mwenyekiti wa Taifa CCM aliongeza kuwa taarifa hiyo ya ajali ambayo imesababisha vifo vya watu wengi imewasikitisha wana-CCM kwa upande wa Zanzibar na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar(SMZ) na kwamba Zanzibar iko pamoja katika kuomboleza msiba huo mkubwa wa taifa.

"Taarifa iliotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Dk.John Magufuli ya uamuzi wa Serikali kuomboleza siku nne ni dhahiri kuwa ni msiba mkubwa kwa Tanzania sisi kwa upande wa Zanzibar tulikuwa na sherehe mbili kubwa tumeziharisha zote kwa kuwa tunaomboleza kwa maagizo ya Rais Dk.Magufuli,"amesema Dk.Shein

Rais Dk.Shein amesema ilitarajiwa kufanywa sherehe kubwa za Elimu bila malipo na kuwatunuku zawadi wanafunzi wa kidato cha sita waliofaulu lakini shughuli hizo zimeaharishwa kutokana na ukubwa jambo hilo.

Dk.Shein ameeleza kuwa sherehe zote zilizotakiwa kufanyika visiwani humu zimeharishwa kutokana na kuwepo kwa msiba huo mkubwa na kwamba Zanzibar inaungana na ndugu na jamaa katika kuomboleza.

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu wa CCM,Zanzibar Dk.Abdulla Saadalla Juma 'Mabodi' kwa niaba ya Kamati hiyo Maalum ya Halmashauri Kuu amesema imetoa shilingi milioni tano kwa ajili ya mchango wa rambirambi wa msiba huo na kwamba kiasi hicho ni cha kuanzia.

Alisema CCM kwa upande wa Zanzibar ina ungana na wafiwa wote wa msiba huo na kwamba chama kitaendelea kutoa mchango wake kadri mahitaji yatakapohitaji.

"Kabla ya kuanza kikao chetu tumefungua kwa dua ya kuwaombea waliofariki katika ajali hiyo na hatujaishia hapo tumetoa tamko rasmi la kuhusu msiba huu kwa ujumla tunawapa pole na tunawaomba kuwa na subira katika kipindi hiki kigumu,"alisema Dk.Mabodi

Katika maelezo yake Naibu Katibu Mkuu huyo ameleeza kwamba CCM kwa upande wa Zanzibar inawaomba watanzania kutotumia msiba huo kwa kuwagawa wananchi kisiasa na hivyo wanatakiwa kuwa wamoja.

Amesema Kamati Maalum inawaomba wanafamilia,ndugu na jamaa wa marehemu na majeruhi katika ajali hiyo kuendelea kuwa na hali ya subira wakati wa kipindi hicho cha msiba huo mkubwa.

"CCM kinaamini kuwa Serikali itafanya uchunguzi wa kina wa tukio hili ili kubaini kilichotokea na kwamba watebdaji wetu watakwenda kuungana na viongozi wenzetu huko Tanzania bara katika kusaidia kuungana kuomboleza,"ameeleza Dk.Mabodi

Ajali hiyo imetokea Septemba 20 mwaka huu katika majira ya saa 6 mchana katika ziwa Victoria wakati ikiwa kwenye safari yake ya kutoka Bugorola kuelekea kisiwa cha Ukara.

Mbali na hilo, Naibu huyo Katibu Mkuu amefafanua kuwa katika kikao hicho cha kamati Maalum ya Halmashauri kuu kilichokutana mjini Unguja pia kimewajadili wagombea watatu wa nafasi ya uwakilishi jimbo la Jangombe katika uchaguzi mdogo unaotarajiwa kufanyika Oktoba 27 mwaka huu.

Dk.Mabodi amesema  baada ya wajumbe wa kamati hiyo kuwapa alama wagombea hao ndipo majina hayo yatapelekwa Kamati Kuu kwa ajili ya kuchagua jina moja litakalopeperusha bendera ya CCM katika uchaguzi huo.

Pia ameeleza kuwa maandalizi ya kampeni katika jimbo hilo la Jangombe yako vizuri na kwamba CCM itashinda kwa asilimia kubwa kwenye uchaguzi huo.  

Wakati huo huo, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan amekabidhi mabati 180 kwa Naibu Katibu Mkuu wa CCM,Zanzibar Dk.Abdulla Saadalla Juma 'Mabodi' ikiwa sehemu ya utekelezaji wake wa ahadi aliyotoa katika ziara yake ya Kichama aliyofanya miezi kadhaa iliyopita huko katika Tawi la CCM Urusi Jang'ombe.

Makamu huyo wa Rais amesema katika ziara yake ya kichama Pemba na Unguja matawi mengi ya vijijini na mjini waliomba msaada wa mabati hayo kwa ajili ya kuyaweka katika matawi hayo.

Maoni 1 :

  1. Hongera Sana chama cha Maoinduzi pamoja na hayo pia Tutakapo chagua mgombea tuchaguwe makini na awe nadifa kamili ili tusijefanya tena kosa lililotokea

    JibuFuta