Jumanne, 4 Septemba 2018

THUWAYBA: AHIMIZA MSHIKAMANO

 MAKAMU Mwenyekiti wa UWT Taifa, Thuwayba Kisasi akizungumza katika moja ya Mkutano wa UWT uliofanyika katika ukumbi wa Wilaya ya Amani, Unguja.


MAKAMU Mwenyekti wa Umoja wa Wanawake (UWT) wa Taifa, Thuwayba Edington Kisasi amewataka akina mama kuepuka migawanyiko na makundi ndani ya CCM na badala yake kushirikiana katika kukijenga na kukiimarisha chama hicho.


Kisasi ameeleza hayo huko kwenye mkutano wa Baraza la Umoja wa Wanawake (UWT), wilaya ya Amani alipokuwa akifungua mkutano na akinamama wa Jumuiya hiyo.


Amesema iko haja ya kukemewa kuwepo kwa makundi ndani ya jumuiya hiyo, kwani hilo ni tatizo kwa Chama cha Mapinduzi na kwamba chama kinapomaliza uchaguzi kiungane kuwa kitu kimoja.


“Upo mtandao unaoendeleza migawainyiko na makundi ndani chama na jumuiya, lakini niwahakikishie kuwa hatua zitachuuliwa kwa wahusika wote waliounda makundi hayo”, alisema Makamu huyo.


Amewataka akinamama wajitambue thamani yao kwa kuwa ni tegemeo kubwa kwa CCM, familia na jamii, hivyo kanuni za chama hicho ziendelezwe hali ambayo itakifanya kiimarike zaidi.


Amewahimiza wanawake hao kujishughulisha na miradi ya maendeleo ambayo itawawezesha kujipatia kipato, hali itakayowaepusha na utegemezi hasa ikizingatiwa kuwa fursa za kujikomboa zipo.


Thuwaiba amekemea vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia kwa wanawake na watoto na kuwataka akina mama kuhakikisha wanazidisha uangalizi kwa watoto na kuviripoti kwenye vyombo vya sheria ili wahusika wachukuliwe hatua.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni