Jumamosi, 14 Julai 2018

" VIONGOZI JIPIMENI KATIKA UTENDAJI WENU WA KAZI " ND. BAKARI

Katibu wa Oganization  CCM Zanzibar Nd. Bakari  akizungumza na wanaCCM wa Tawi la Shaurimoyo ' B'


CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), Zanzibar, kimewataka viongozi wa wa chama visiwani humu kujipima katika utendaji wao wa kutoa huduma kwa wananchi. 

Kauli hiyo ameitoa Katibu wa Kamati Maalum ya NEC, Idara ya Organaizesheni,Zanzibar,Bakari Hamad Khamis wakati akizungumza wanachama wa tawi la Shauri Moyo 'B', mjini Unguja alisema endapo inaridhisha iongezwe juhudi zaidi.

Alisema na kama viongozi hao utendaji wao haujiridhishi inapaswa kujiuliza sababu ambazo zinasababisha kutofanikiwa kufikia malengo yaliowekwa. 

"Lakini si viongozi pekee bali wanachama wote tunawajibika kufanya kazi hiyo kwa mantiki ya kuimarisha chama chetu pamoja na kuhudumisha Zanzibar yetu,"alisema Katibu huyo 

 Katika maelezo yake Katibu Bakari alisema wanachama wanatakiwa kuwa wa moja ili kukijenga chama na kwamba endapo wakianza kuunga mkono hoja za wapinzani hivyo kwa kufanya hivyo ni kutoisaidia Serikali ambayo inaongozwa na CCM.

 "Sisi viongozi tunatakiwa tuelewe kuwa ni watu wa kwanza katika kukisimamia chama na kuisimamia Serikali kazi moja ya serikali ni kutekeleza majukumu waliopewa na chama na ndio maana ikifika wakati wa uchaguzi tunaanda ilani,"alisema Katibu huyo 

 Aliongeza kuwa lazima wanachama wae na umoja ili kuhakikisha chama kinabaki kuendelea kushika dola na kuwatatulia matatizo wananchi na kuwaletea maendeleo.

Katibu wa Oganization CCM Zanzibar Nd. Bakari akiwasili katika  Tawi la Shaurimoyo ' B' kwa ajili ya kuzungumza na wanachama wa CCM Tawi  hilo

Katibu wa Oganization  CCM Zanzibar Nd. Bakari  akipokea risala kutoka kwa Nd. Arafa Juma Faki 
ambae ni Katibu wa CCM Tawi la Shaurimoyo ' B'

Katibu wa Oganization  CCM Zanzibar Nd. Bakari  akizungumza na wanaCCM wa Tawi la Shaurimoyo ' B'



Kaimu Katibu wa Wilaya ya Amani ambae pia ni Katibu wa Wazazi wilaya ya Amani Nd.Mwanaisha Ame Moh'd akitoa nasaha zake kwa Wanachama hao wa CCM wa Tawi la Shaurimoyo ' B'

Add caption

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni