Alhamisi, 5 Oktoba 2017

MATUKIO KATIKA PICHA UCHAGUZI WA CCM NGAZI ZA WILAYA ZANZIBAR ULIOFANYIKA LEO.

Naibu katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdalla Juma Mabodi akifungua mkutano Mkuu wa CCM Wilaya ya  Kaskazini “A”  kichama katika uchaguzi wa Wilaya  uliofanyika leo katika ukumbi wa CCM MKoa wa kaskazini Unguja Mahonda

Mjumbe wa Kamati kuu ya CCM Taifa, Dk. Hussein Mwinyi akifungua mkutano Mkuu wa CCM Wilaya ya Mjini uliofanyika katika Ukumbi wa Baraza la Wawakilishi la Zamani Kikwajuni Unguja.
 Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM Wilaya ya Kati akipiga kura katika uchaguzi uliofanyika leo huko katika ukumbi wa Skuli ya Dunga.


Baadhi ya wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Wilaya ya Amani wakifuatilia kwa makini harakati mbali mbali zinazofanyika katika uchaguzi huo huko katika Ukumbi wa CCM Mkoa wa Mjini huko Amani Unguja.

Baadhi ya wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Wilaya ya Mjini wakifuatilia kwa makini harakati mbali mbali zinazofanyika katika uchaguzi huo katika Ukumbi wa Baraza la Wawakilishi la Zamani Kikwajuni Unguja.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni