Jumamosi, 14 Julai 2018

" VIONGOZI JIPIMENI KATIKA UTENDAJI WENU WA KAZI " ND. BAKARI

Katibu wa Oganization  CCM Zanzibar Nd. Bakari  akizungumza na wanaCCM wa Tawi la Shaurimoyo ' B'


CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), Zanzibar, kimewataka viongozi wa wa chama visiwani humu kujipima katika utendaji wao wa kutoa huduma kwa wananchi. 

Kauli hiyo ameitoa Katibu wa Kamati Maalum ya NEC, Idara ya Organaizesheni,Zanzibar,Bakari Hamad Khamis wakati akizungumza wanachama wa tawi la Shauri Moyo 'B', mjini Unguja alisema endapo inaridhisha iongezwe juhudi zaidi.

Alisema na kama viongozi hao utendaji wao haujiridhishi inapaswa kujiuliza sababu ambazo zinasababisha kutofanikiwa kufikia malengo yaliowekwa. 

"Lakini si viongozi pekee bali wanachama wote tunawajibika kufanya kazi hiyo kwa mantiki ya kuimarisha chama chetu pamoja na kuhudumisha Zanzibar yetu,"alisema Katibu huyo 

 Katika maelezo yake Katibu Bakari alisema wanachama wanatakiwa kuwa wa moja ili kukijenga chama na kwamba endapo wakianza kuunga mkono hoja za wapinzani hivyo kwa kufanya hivyo ni kutoisaidia Serikali ambayo inaongozwa na CCM.

 "Sisi viongozi tunatakiwa tuelewe kuwa ni watu wa kwanza katika kukisimamia chama na kuisimamia Serikali kazi moja ya serikali ni kutekeleza majukumu waliopewa na chama na ndio maana ikifika wakati wa uchaguzi tunaanda ilani,"alisema Katibu huyo 

 Aliongeza kuwa lazima wanachama wae na umoja ili kuhakikisha chama kinabaki kuendelea kushika dola na kuwatatulia matatizo wananchi na kuwaletea maendeleo.

Katibu wa Oganization CCM Zanzibar Nd. Bakari akiwasili katika  Tawi la Shaurimoyo ' B' kwa ajili ya kuzungumza na wanachama wa CCM Tawi  hilo

Katibu wa Oganization  CCM Zanzibar Nd. Bakari  akipokea risala kutoka kwa Nd. Arafa Juma Faki 
ambae ni Katibu wa CCM Tawi la Shaurimoyo ' B'

Katibu wa Oganization  CCM Zanzibar Nd. Bakari  akizungumza na wanaCCM wa Tawi la Shaurimoyo ' B'



Kaimu Katibu wa Wilaya ya Amani ambae pia ni Katibu wa Wazazi wilaya ya Amani Nd.Mwanaisha Ame Moh'd akitoa nasaha zake kwa Wanachama hao wa CCM wa Tawi la Shaurimoyo ' B'

Add caption

Jumatatu, 9 Julai 2018

MAMA SAMIA AONGOZA KIKAO CHA KAMATI MAALUM YA HALMASHAURI KUU YA CCM TAIFA ZANZIBAR


MJUMBE wa Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambaye pia ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo Julai 9, mwaka 2018 ameongoza Kikao cha Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Zanzibar.

Makamu wa Rais Mhe. Samia ameongoza kikao hicho baada ya kupendekezwa na wajumbe wa kikao kwa mujibu wa Katiba ya CCM, Ibara ya 108 (4) ili aongoze kikao hicho kwa niaba ya Makamu Mwenyekiti wa CCM Dk. Ali Mohamed Shein aliyesafiri nje ya nchi kikazi. 

 Kikao hicho kimefanyika kuanzia majira ya saa 4:00 asubuhi hadi saa 7:30 mchana katika ukumbi wa Mikutano wa Afisi Kuu ya Chama Cha Mapinduzi, Kisiwanduzi Zanzibar.

Pamoja na mambo mengine kikao hicho kilikuwa na ajenda moja ya kujadili kwa kina majina 19 ya Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi waliojitokeza kugombea nafasi ya uwakilishi katika jimbo la Jang’ombe Zanzibar. 

 Wanachama hao 19 walioomba nafasi hiyo na kupendekezwa katika ngazi za jimbo, wilaya na Mkoa, Kikao hicho kimeweka alama zinazostahiki kwa wagombea wote na kupendekeza kwa Kamati Kuu ya CCM Taifa ili irejeshe majina matatu au kama itakavyoona inafaa kwa ajili ya kura ya maoni kwa lengo la kumpata mgombea mmoja atakayepeperusha bendera ya CCM katika Uchaguzi mdogo wa jimbo hilo. Kikao hicho ni maalum kwa mujibu wa Katiba ya CCM ya mwaka 1977 toleo la 2017, ibara ya 109 (1) na 7(b).

 Mchakato huo unafanyika kutokana na Jimbo la Jang’ombe kuwa wazi baada ya aliyekuwa Mwakilishi wa Jimbo hilo Abdalla Diwani kufukuzwa uanachama wa CCM hivi karibuni baada ya kukiuka maadili na miongozo ya Chama.

  MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa Mhe. Samia Suluhu Hassan (kushoto) akisalimiana na Wajumbe wa Kamati Maalum ya NEC Taifa Zanzibar  kilichofanyika leo  katika ukumbi wa Afisi Kuu CCM Kisiwandui.

 
 MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa Mhe. Samia Suluhu Hassan  akiingia Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui Zanzibar kwa ajili ya kuongoza kikao cha NEC Taifa Zanzibar.
BAADHI ya Wajumbe wa Kikao hicho 

 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk. Abdulla Juma Saadalla Mabodi akisoma ajenda za Kikao cha Kamati Maalum ya NEC Taifa Zanzibar cha kujadili majina ya Wana CCM waliowania kugombea nafasi ya uwakilishi jimbo la Jang'ombe.

WAGOMBEA 19 wa CCM wanaowania nafasi ya uwakilishi wa Jimbo la Jang'ombe wakiwa katika picha ya Pamoja.