MAKAMU Mwenyekiti wa CCM, Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein, kesho
(24/03/2017) anatarajia kukiongoza kikao cha Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu
(NEC) ya Taifa ya CCM Zanzibar.
Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari
iliyotolewa na katibu wa Kamati Maalum ya NEC wa Idara ya Itikadi na Uenezi
Mhe. Waride Bakari Jabu, amesema kikao hicho maalum cha siku moja kitafanyika Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui.
Amesema kwa kuwa kikao hicho ni maalum, kitakuwa na agenda
moja tu, ambayo ni kupokea na kujadili majina ya wana CCM waliojitokeza
kuchukua fomu za kugombea nafasi ya Ubunge
wa Bunge la Afrika Mashariki.
Kwa mnasaba huo, Katibu huyo wa Kamati Maalum ya NEC
Zanzibar amewataka Wajumbe wote wa kikao hicho kuwa wameshakaa kwenye viti vyao
ifikapo saa 3:30 barabara za asubuhi.
Kikao hicho kilitanguliwa na kikao cha Sekretarieti ya
Kamati Maalum ya NEC Zanzibar, iliyokutana leo
(23/03/2017) chini ya Mwenyekiti wake Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar
Mhe. Abdullah Juma Abdullah (Mabodi) kwa ajili ya kuandaa ajenda ya kikao
hicho.
KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI
(Waride Bakari Jabu),
Katibu wa Kamati Maalum ya NEC,
Idara ya Itikadi na Uenezi,
ZANZIBAR.
23/03/2017.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni