Jumamosi, 6 Juni 2015

Wanawake wamepongezwa kwa kutumia nafasi iliopo katika katiba

Mhe. Vuai Ali Vuai akisalimiana na Mhe. Amina Salum Ali, Hapo Afisi Kuu CCM - Zanzibar


Mhe. Amina akisaini katika kitabu ambacho wageni huwa wanasaini pindi tu wanapofika hapo

Mhe. Naibu Katibu Mkuu akitoa nasaha kwa Mgombea ambae aliyefika hapo Afisi Kuu CCM - Zanzibar kwa ajili ya kusalimiana nae

Mhe. Amina Salum Ali akizungumza na waandishi wa habari hapo katika Afisi Kuu CCM - Zanzibar
Wanawake wamepongezwa kwa kutumia nafasi iliopo katika katiba ya kuwania nafasi za juu za uongozi kwa ajili ya kuleta mabadiliko na maendeleo katika taifa.

Hayo yalisemwa na Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Zanzibar Vuai Ali Vuai wakati akisalimiana na mgombea wa nafasi ya urais wa Jamhuri ya Muungano aliyechukuwa fomu kuwania kinyanganyiro hicho Amina Salum Ali ambaye alifika Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui kwa ajili ya kujitambulisha.

Alisema
Chama Cha Mapinduzi ni miongoni mwa taasisi zenye demokrasia pana ya kutoa nafasi kwa viongozi wake katika makundi mbali mbali kuchukuwa fomu na kuwania nafasi za juu za uongozi bila ya vikwazo.

'Kwa niaba ya
Chama Cha Mapinduzi tunakupongeza kwa kuamuwa kujitokeza kuchukuwa fomu ya urais wa Zanzibar hatua ambayo inadhihirisha mshikamano uliopo ndani ya chama na nafasi yake kwa watu mbali mbali kuwania nafasi za uongozi bila ya vikwazo'alisema.

Mapema Amina alikipongeza
Chama Cha Mapinduzi kwa demokrasia yake iliopo ambayo imetoa nafasi kubwa kwa wanwake kugombea nafasi mbali mbali za juu za uongozi.

Alisema ameamuwa kuchukuwa fomu kuwania nafasi ya juu ya uongozi katika chama cha Mapinduzi kwa ajili ya kutimiza matakwa ya demokrasia iliopo ndani ya chama ambayo ni kubwa.

'Nakipongeza Chama Cha Mapinduzi kwa kujenga demokrasia pana ambayo leo hii imeniwezesha kuchukuwa fomu kuwania nafasi ya juu ya urais wa muungano'alisema.

Aliwataka wanawake wenzake kuitumia fursa ya demokrasia iliopo katika
Chama Cha Mapinduzi ambayo ni ya kupigiwa mfano yenye malengo ya kuzishirikisha jinsia zote katika uongozi wa nchi.

Mapema Amina alifika katika afisi kuu ya CCM Kisiwandui na kupokewa na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai na kutoa salamu zake za shukrani kwa chama cha Mapinduzi kwa kumpa kila aina ya ushirikiano.

Mgombea huyo alisema ameanza safari ya kutembea mikoa ya Tanzania ikiwemo Pemba kwa ajili ya kusaka wadhamini ambao watamuwezesha kukamilisha masharti ya fomu ya kuwania nafasi ya urais.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni