Jumamosi, 3 Machi 2018

DK.MABODI-AWATAKA WANANCHI KUJIUNGA NA VIKUNDI VYA UJASIRIA MALI

 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar akihutubia katika hafla ya maonyesho ya  wajasiriamali iliyofanyika huko Fuoni Skuli Zanzibar.

Naibu Katibu Mkuu CCM Zanzibar Dk.Mabodi awataka wajasiri wa Jimbo la Dimani kujinga na wajasiriamali kutoka sehemu mbali mbali za Dunia ili wapate ujuzi wa kutengeneza bidhaa bora zinazokubalika katika masoko ya biashara ya ndani na nje ya nchi.

Wito huo ameutoa leo wakati akizungumza na wajasiria mali hao huko Viwanja vya Skuli ya Fuoni  Unguja, amesema endapo wajasiriamali hao watatengeneza bidhaa bora watakuwa wamefungua fursa ya bidhaa zao kuongezeka thamani na kukunuliwa kwa wingi.


Amesema njia pekee ya kuongeza ubunifu katika utengenezaji wa bidhaa hizo kwa wajasiriamali hao ni kujifunza ubunifu kutoka kwa wenzao wenye uzoefu mkubwa wa utengenezaji wa bidhaa hizo kwa lengo la kujiongeza kibiashara na kuingiza kipato cha uhakika.

"Nimefurahi sana kuona baadhi ya bidhaa zetu za ndani zinawekwa katika vifungashio kwa kisasa na zinakuwa na muonekano mzuri ambao ni moja ya kivutio kikubwa katika masoko ya kimataifa",amewapongeza Wajasiriamali hao Dk.Mabodi.

Ameeleza kuwa huwezi kuzungumzia maendeleo katika nchi zilizostawi kiuchumi bila kutaja mchango wa Sekta ya ujasiriamali inayoingiza fedha nyingi kutoka katika mzunguko wa biashara na masoko.

Pamoja na hayo aliwambia wananchi kupitia hafla hiyo kuwa fursa hizo zinatokana na usimamizi mzuri wa Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015/2020 inayotekelezwa na Serikali zote mbili ya  Jamhuri ya Muungano inaongozwa na Dkt. Magufuli  na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ambayo inaongozwa na Dk. Ali Mohamed Shein .

 Amesema serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ina dhamira ya kuendelea kuimarisha ustawi wa vijana kwa kuwapatia mafunzo mbali mbali ya stadi za maisha ili wawe na ujuzi utakaowawezesha kujiajili wenyewe.

Pia ametoa wito kwa wananchi mbali mbali kuvisajili vikundi vyao kupitia utaratibu unaotambuliwa kisheria ili wanufaike  na huduma ya  mikopo yenye masharti nafuu  kupitia mfuko wa uwezeshaji.

Dk. Mabodi akisalimiana na Viongozi mbali mbali wa Chama na Serikali mara tu baada ya kuwasili katika Viwanja vya Skuli ya Msingi Fuoni kwa lengo la kukutana na wajasiriamali wa Jimbo la Dimani

Mbunge wa Dimani Ndg, Juma Ali Juma akimuonesha Dk. Mabodi moja ya bidhaa ambazo zinafanywa na
 wajasiriamali  wa Jimbo la Dimani

Dk. Mabodi akipata malezo kutoka kwa mmoja kati ya wakufunzi Ndg, Fuadi

Naibu akizidi kukagua bidhaa za wajasiriamali hao

Dk. Mabodi akipokea zawadi aliyotunukiwa na wajasiri amali hao kutoka Dimani

Dk. Mabodi akitizama kwa bashasha moja kati ya zawadi aliyotunukiwa na wajasiri amali hao kutoka Dimani

Dk. Mabodi akisalimiana na mmoja kati ya washirika wa maendeleo kutoka Canada

NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar akiwa katika picha ya pamoja na Wasiriamali na viongozi mbali mbali wa CCM Wilaya ya Dimani.

Alhamisi, 1 Machi 2018

CCM ZANZIBAR YATOA AGIZO ZITO KWA VIONGOZI WA CHAMA NA SERIKALI

KATIBU wa Kamati Maalum ya NEC, Idara ya Ikadi na Uenezi CCM Zanzibar, Bi, Catherine Peter Nao akizungumza mara baada ya kuwasili katika studio za Swahiba Fm iliyopo Mbweni Zanzibar.

 Mkurugenzi wa Swahiba Fm, Maalim Kassim Mohamed Kassim(kulia) akizungumza na Katibu wa Kamati Maalum ya NEC, Idara ya Itikadi na Uenezi CCM Zanzibar Ndugu Catherine Peter Nao mara baada ya kuwasili katika Kituo cha radio hiyo kwa ajili ya kujitambulisha.

 WAFANYAKAZI wa Swahiba Fm wakiwa katika picha ya pamoja na wageni wao kutoka Afisi Kuu CCM Zanzibar wakiongozwa na Katibu wa Kamati Maalum ya NEC, Idara ya Itikadi na Uenezi CCM Zanzibar Ndugu Catherine Peter Nao.

 KATIBU wa Kamati Maalum ya NEC, Idara ya Itikadi na Uenezi CCM Zanzibar Ndugu Catherine Peter Nao akizungumza mara baada ya kuwasili katika studio za Chuchu FM iliyopo Mlandege Zanzibar.

 MKUU wa Vipindi Chuchu Fm, Mulhat Doria(wa kwanza kulia aliyevaa mtandio wa rangi nyekundu) akizungumza na ujumbe wa ugeni huo kutoka CCM Zanzibar.

 Mhariri Mtendaji wa Magazeti ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dkt. Yussuf Khamis Yussuf(wa kwanza kushoto) akizungumza na Katibu  wa Kamati Maalum ya NEC, Idara ya Itikadi na Uenezi CCM Zanzibar Ndugu Catherine Peter Nao alipofika ofisini kwake Maisara kwa ajili ya kujitambulisha. 
 Mhariri wa Zanzibar leo Juma Khamis (aliyesimama akizungumza mwenye shati la mistari) akiwatambulisha wafanyakazi wa Shirika la Magazeti ya Serikali Zanzibar waliokuwepo katika Chumba cha Habari baada ya kutembelewa na Katibu wa Kamati Maalum ya NEC, Idara ya Itikadi na Uenezi CCM Zanzibar Ndugu Catherine Peter Nao.

 MKUU wa Waandishi wa habari Zanzibar leo Ndugu Mwantanga Ame (kulia) awakionyeshwa machapisho mbali mbali ya Gazeti la Zanzibar leo Toleo la No.5804 la Machi 1, 2018 Katibu wa Kamati Maalum ya NEC, Idara ya Itikadi na Uenezi CCM Zanzibar Ndugu Catherine Peter Nao (kushoto) na Katibu msaidizi wa Idara hiyo Daud Ismail Juma(wa pili kushoto).


NA IS-HAKA OMAR, ZANZIBAR.


TASNIA ya Habari ni sekta muhimu inayoziwezesha Serikali mbali mbali Duniani kuimarisha dhana ya Demokrasia kupitia matangazo na taarifa za utekelezaji wa Ilani ya Chama tawala, miongozo na mipango ya maendeleo ili wananchi wajue uwajibikaji wa serikali yao na kupima uhalisia wa sera zinazotekelezwa kama zinakidhi mahitaji yao.


Maelezo hayo yametolewa na Katibu wa Kamati Maalum ya NEC, Idara ya Itikadi na Uenezi CCM Zanzibar Bi. Catherine Peter Nao katika mwendelezo wa ziara yake katika vyombo Zanzibar, kutokana na umuhimu wa sekta hiyo Katibu huyo ameagiza viongozi na watendaji wa Chama na Serikali kupanga utaratibu wa   kuzungumza na vyombo vya Habari mara kwa mara  ili waweze kuwaeleza wananchi utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku katika taasisi zao.


Catherine amesema  kiongozi yeyote mwenye dhamana ya kutoa taarifa za Chama ama Serikali atakayekataa kuzungumza na vyombo vya habari atakuwa anaenda kinyume na falsafa ya CCM mpya na Tanzania mpya inayotaka Chama kirudi mikononi mwa wananchi kwa kuanza na hatua ya kuwapatia taarifa sahihi zinazohusu masuala ya maendeleo.


Amesema kiongozi anayetekeleza wajibu wake vizuri hawezi kuwa na hofu ya kuzungumza na vyombo vya habari, hivyo ni lazima watumishi hao wa umma kukubali mabadiliko ya zama mpya za utandawazi zinazotoa fursa ya wananchi kuhoji na kudadisi viongozi waliowapa dhamana nini wamefakanya katika maeneo yao.


“Serikali ya Mapiunduzi ya Zanzibar chini ya uongozi wa Dk. Ali Mohamed Shein imefanya mambo mengi mazuri lakini cha kusikitisha wananchi wengi hawajui serikali yao nini inafanya kutokana na baadhi ya Viongozi wenye dhamana ya kuzungumza wapo kimya”, alisema Catherine.


Agizo hilo limetolewa baada ya Vyombo vya Habari mbali mbali nchini kulalamikia urasimu usikuwa na tija wa baadhi ya Viongozi na Watendaji wa Chama na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, kutotoa ushirikiano kwa taasisi za kihabari hali inayosababisha baadhi ya vyombo hivyo kutoa taarifa za upande mmoja baada ya kukosekana ushirikiano kutoka kwa viongozi wa umma.


Pia amewapongeza Mwenyekiti wa CCM Taifa Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein kwa juhudi zao za kusimamia na kutekeleza ilani ya CCM kwa kasi kubwa hatua inayoleta furaha ya kudumu kwa wananchi.


Hata hivyo Katibu huyo amesema  licha ya kuwepo na changamoto mbali mbali za kiutendaji bado CCM inaendelea kubaki katika msimamo wake kwa mujibu wa Ibara ya tano ya Katiba ya CCM ya mwaka 1977 kwa kuhakikisha mwaka 2020 CCM inashinda katika Uchaguzi wa ngazi zote  na kubaki madarakani.


Ameeleza kuwa  lengo la ziara hiyo ni kujitambulisha kwa vyombo hivyo ambavyo ni wadau wakubwa wa Chama Cha Mapinduzi ili waweze kufanya kazi kwa ushirikiano kwa maslahi ya wananchi.


Akizungumza Mkurugenzi wa Swahiba FM Radio, Maalim Kassim Mohamed Kassim alisema Vyombo vya habari vipo kwa ajili ya wananchi hivyo kiongozi yeyote aliyepewa dhamana na wananchi ana wajibu wa kutoa ushirikiano kwa taasisi hizo.


Mkurugenzi huyo amekishauri Chama Cha Mapinduzi kukaa pamoja na viongozi wa Serikali hasa mawaziri na wakurugenzi kuwasihi watoe ushirikiano kwa kituo chake pindi wanapohitajika kwa ajili ya kutoa ufafanuzi wa masuala mbali mbali ya kijamii, kisiasa na kiuchumi.


Naye Mhariri Mtendaji wa Shirika la Magazeti ya Serikali Zanzibar, Yussuf Khamis Yussuf amesema Shirika hilo litaendelea kutoa habari mbali mbali zinazohusu utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015/2020, huku wakizingatia kanuni na miongozi ya maadili ya Tasnia ya habari.


Naye Meneja wa Chuchu Fm Salma Ahmed Alley, amesema pamoja juhudi za taasisi hiyo katika    kuelimisha, kuhabarisha, kukosoa na kuhamasisha amani na utulivu bado wanakabiliwa na  changamoto ya ukosefu wa matangazo ya biashara kutoka Serikalini na taasisi zingine hali inayosababisha baadhi ya wakati chombo hicho kuyumba kifedha.



Pamoja na hayo Salma amesifu juhudi za  Katibu huyo wa Idara ya Itikadi na Uenezi CCM Zanzibar Bi. Catherine kwa ujasiri wake wa kuvithamini vyombo vya habari na kufungua milango ya ushirikiano wa kudumu.