Jumamosi, 21 Desemba 2019

MHE.ASHA AKING'ARISHA KITUO CHA UJASIRIAMALI CHA UWT


MBUNGE wa Viti Maalum Mkoa wa Mjini Mhe.Asha Abdulla Juma akikabidhi Vifaa vikiwemo vitambaa pamoja na Vyerehani kwa Mwenyekiti  wa Umoja wa Wanawake Tanzania Wilaya ya Mjini Habiba Nassib Suleiman kwa ajili ya Kituo cha Elimu Amali UWT Wilaya ya Mjini.

MBUNGE wa Viti Maalum Mkoa wa Mjini Mhe.Asha Abdulla Juma akizungumza na Viongozi wa Umoja wa Wanawake Tanzania Wilaya ya mjini wakati wa hafla ya makabidhiano ya vifaa mbalimbali kwa ajili ya kituo cha elimu amali UWT wilaya ya mjini iliyofanyika katika kituo hicho Mwembe Matumbaku Wilaya ya Mjini unguja.

MWENYEKITI wa UWT Wilaya ya Mjini Ndugu Habiba Nassib Suleiman akimkabidhi zawadi maalum Mbunge wa Viti Maalum  Mkoa wa Mjini Mhe.Asha Abdulla Juma katika hafla ya kukabidhi msaada wa vifaa mbalimbali kwa kituo cha elimu amali UWT wilaya ya mjini iliyofanyika katika ukumbi wa chuo hicho mwembe matumbaku wilaya ya mjini unguja.

katibu wa UWT wilaya ya Mjini akizungumza na baadhi ya viongozi na wa jumuiya hiyo wakati wa makabidhiano ya vifaa mbalimbali kwa ajili ya kituo cha elimu amali UWT wilaya ya mjini uliotolewa na mbunge wa viti maalum ccm mkoa wa mjini Asha Abdulla Juma.





MBUNGE wa viti maalum wa Mkoa wa Mjini,Mhe Asha Abdulla Juma amefurahishwa na hatua ya Jumuiya ya Wanawake Tanzania (UWT) ya Chama Cha Mapinduzi ya wilaya ya Mjini kutekeleza kwa vitendo ilani ya uchaguzi kwa kuhakikisha vijana wanajikwamua kiuchumi.

Amesema kitendo cha UWT kuwakusanya vijana tofauti ndani ya mkoa huo kwa lengo la kuwapatia mafunzo ya ujasiriamali ili waweze kuondokana na hali ya utegemezi ambapo baadaye wakipata ujuzi wanajishughulisha na uzalishaji wa bidhaa mbalimbali ili kujiingizia kipato ni moja ya sehemu ya maagizo ya ilani pamoja na viongozi wa chama.

Kauli hiyo ameitoa wakati akikabidhi vifaa vya ushonaji ikiwemo chereheani mbili,meza pamoja na vitambaa vya kutengeneza mapambo katika kituo cha mafunzo ya amali cha UWT wilaya ya mjini ambapo alisema hiyo ni ahadi za CCM katika kuwakusanya vijana na kuwajengea uwezo wa kujitegemea na kuondokana na utegemezi.

Amesema baada ya kuona Jumuiya hiyo imeanzisha kituo hicho cha mafunzo kwa ajili ya vijana akaiona aunge mkono juhudi hizo za kuhakikisha vijana hao wanaokombolewa dhidi ya ukosefu wa ajira ili kuongeza uzalishaji nchini kama maagizo ya viongozi wa CCM wanavyoelekeza.

"Nina amini chuo hichi kitasaidia sana juhudi hizi kwa vijana wetu na ndio maana nikaona nilete nguvu kwenye kituo hichi cha UWT hasa kwa wakina mama katika kujifunza ujasiriamali wa ushonaji,upishi na mambo mengine,"ameeleza

Naye Mwenyekiti wa UWT wilaya ya Mjini,Habiba Nassir Suleiman amesema lengo la uongozi wa wilaya hiyo ni kuendelea  kubuni miradi itakayosaidia kuondoa tatizo la ukosefu wa ajira na ongezeko la uzalishaji kwa lengo la kukuza uchumi kama inavyoelekeza CCM.

Amesema uongozi wa UWT wilaya imeamua kufanya ubunifu wa aina hiyo wa kuwakusanya vijana na kuwapatia mafunzo ya ujuzi wa shughuli za ujasiriamali ambapo kwa namna moja ama nyingine itawasaidia sana wanawake katika kuondokana na hali ya utegemezi na kuweza kujikwamua kiuchumi.








Hakuna maoni:

Chapisha Maoni