Jumamosi, 29 Juni 2019

MHE.ASHA 'MSHUA'- ATAKA WANAWAKE WAWE CHACHU YA USHINDI 2020,ATOA VITENDEA KAZI TSH.MILIONI 1.5

MBUNGE wa Viti Maalum Mkoa wa Mjini Mhe.Asha Abdalla Juma "Mshua' na Katibu wa UWT Wilaya ya Amani Ndugu Asha Mzee wakiwa wamebeba Vitendea kazi vilivyotolewa na Mhe.Asha kwa ajili ya kufanikisha kazi za UWT.

  MBUNGE wa Viti Maalum Mkoa wa Mjini Mhe.Asha Abdalla Juma "Mshua',akikabidhi Vitendea kazi kwa Katibu wa UWT Wilaya ya Amani Ndugu Asha Mzee ambavyo ni Komputa Moja na Printer Moja ya Kisasa vyenye Thamani ya Shilingi Milioni 1.5

 BAADHI ya Wajumbe wa Baraza la UWT Wilaya ya Amani wakisikiliza nasaha za Mgeni rasmi, ambaye ni Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mjini Mhe.Asha Abdalla Juma "Mshua' 


KATIBU wa CCM Wilaya ya Amani Ndugu Ali Salum Suleiman akitoa shukrani kwa Mbunge wa Viti Maalum wa Mkoa wa Mjini Mhe.Asha Abdalla Juma na kuahidi kuwa miongozo aliyotoa kupitia hotuba yake itafanyiwa kazi kwa Vitendo. 


MBUNGE wa Viti Maalum Mkoa wa Mjini Kichama Mhe.Asha Abdalla Juma ‘Mshua’,amewataka Wanawake katika Nchini kuamini,kulinda na kuipigania CCM na kuhakikisha inashinda kwa kishindo mwaka 2020 kuliko Chaguzi zote zilizopita toka kuanzishwa Mfumo wa Vyama Vingi Mwaka 1992.

Amesema Serikali za Awamu ya Saba ya Zanzibar pamoja na Serikali ya Awamu ya Tano ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini wa Marais wake ambao ni Dk.Ali Mohamed Shein na Dkt.John Pombe Magufuli Viongozi waliosimamia Vyema utekelezaji wa Ilani ya CCM.

Hayo ameyasema leo wakati akihutubia katika ufunguzi wa Baraza la UWT Wilaya ya Amani kilichofanyika katika Ofisi za Wilaya hiyo Sebleni Amani Unguja.

Mhe.Asha amesema Serikali hizo zimeimarisha Huduma za Afya,Miundombinu ya Barabara,Umeme,Elimu,Mikopo kwa Wanawake yenye masharti nafuu pamoja na kutoa fursa za  Uongozi kwa Wanawake katika Chama na Serikali zote mbili.

Amesema Wanawake wanatakiwa kuunganisha nguvu zao bila ya kujali bila ya kujali tofauti za Vyeo,rangi na kabila wahakikishe CCM inashinda kwa ngazi zote katika Uchaguzi Mkuu ujao, hiyo ndio itakuwa njia pekee ya kuthamini kwa vitendo juhudi zinazofanywa na Serikali.

Kupitia Mkutano huo amewasihi Wajumbe hao kuendeleza Umoja na Mshikamano katika kutekeleza majukumu yao ya kisiasa ndani na nje ya UWT, kwa lengo la kuandaa mazingira rafiki ya kisiasa yatakayoimarisha CCM.

Amesema pamoja na majukumu waliyokuwa nayo Akina Mama hao pia wanatakiwa kuwalea Watoto katika Maadili mema na kuhakikisha Wanakua Salama bila kufanyiwa Vitendo vya Udhalilishwaji.

Akizungumzia suala Uimarishaji wa Chama na Jumuiya hiyo, Mhe.Asha amesisitiza umuhimu wa kuongeza Wanachama Wapya wenye Sifa kisheria za kuipigia kura CCM kwa kila Uchaguzi wa Dola.

“Kila Mwanachama kwa nafasi yake aanze kuwatafuta Wapiga kura Wapya wa makundi yote wenye Sifa za kupiga kura, waelezeni mazuri mengi yanayopatikana ndani ya CCM japokuwa mengi wanayaona na kuyatambua lakini bado tuna jukumu la kuwakaribisha kwa ukarimu kwani CCM ni Chama cha Wote,,,Nyumbani kumenoga.”,amesema Mhe.Asha.

Kupitia Kikao hicho Mhe.Asha,alikabidhi Komputa Moja na Printer Moja ya Kisasa ya rangi zenye Thamani ya Shilingi Milioni 1.5 kwa Uongozi wa UWT Wilaya hiyo ili watekeleze kwa ufanisi shughuli mbali mbali za kiutendaji.  

Naye Katibu wa UWT Wilaya hiyo Ndugu Asha Mzee,akisoma taarifa ya Utendaji wa kazi za UWT, alisema Viongozi,Watendaji na Wanachama wanashirikiana vizuri huku wakijipanga vizuri kukabiliana na dalili zozote za upinzani ili CCM ishinde katika uchaguzi ujao.

Amesema katika mikakati ya kuimarisha Jumuiya wamesimamia vizuri vikao vya ngazi za Matawi hadi Wilaya kuhakikisha vinafanyika kwa mujibu wa Katiba sambamba na kufanya ziara,vikao na mafunzo ya kuwajenge uwezo Akina Mama juu ya masuala mbali mbali ya kisiasa na kujikwamua kiuchumi.

Akizungumza Mjumbe wa Mkutano huo ambaye pia ni Naibu Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe.Mgeni Hassan Juma, aliupongeza Uongozi wa Wilaya hiyo kwa kutekeleza masuala ya msingi ya kiutendaji yenye dhamira ya kuimasha UWT na Chama Cha Mapinduzi kwa ujumla.

Kwa upande wake Mjembbe wa Mkutano huo ambaye pia ni Mwakilishi wa Viti Maalum kupitia Mkoa huo Mhe.Saada Ramadhan Mwendwa amesema Mkutano huo ulioambatana na Utoaji wa Mada mbali mbali za kuwajengea uwezo Viongozi wa Baraza hilo ili wakirudi katika maeneo yao watekeleze kwa ufanisi majukumu yao.



  

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni