Alhamisi, 4 Julai 2019

WAZEE WA CCM ZANZIBAR WASOMA HITMA YA DK.BADRIYA.


 BAADHI ya Viongozi na Wazee wa CCM Zanzibar wakiwa katika Kisomo cha Hitma ya Mke wa Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Badriya Abubakar Gurnah, kilichoandaliwa na Baraza la Wazee wa CCM Zanzibar na kimefanyika Nyumbani kwake Naibu Katibu Mkuu CCM Zanzibar Rahaleo Unguja.


NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Mabodi, akitoa shukrani kwa Wananchi na Wazee wa CCM walioudhuria Kisomo hicho cha Hitma ya Marehemu Dk.Badriya.
BAADHI ya Viongozi na Wazee wa Chama Cha Mapinduzi kwa upande wa Wanawake walioshiriki katika Kisomo cha Hitma hiyo ya Marehemu Dk.Badriya.


 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Mabodi,akipewa mkono wa pole na Wazee mbali mbali wa Chama mara baada ya Kisomo hicho.


WAZEE wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar pamoja na Viongozi na Wananchi mbali mbali wameungana kusoma Hitma ya Mke wa Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Badriya Abubakar Gurnah.  

Kisomo hicho kilichoandaliwa na Wazee wa Chama kimeudhuriwa na Viongozi na Watendaji wa Serikali,Chama na Jumuiya zake pamoja  Wananchi kwa ujumla.

Akitoa Shukurani zake Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Mabodi,amewashukuru Wazee hao na Wananchi mbali mbali kwa mchango walioutoa kabla na baada ya Msiba huo.

Kwa upande wa Wazee hao wametoa pole kwa Familia ya Dk.Mabodi na kuwasihi waendelee kuwa na subri huku wakiungana na Wananchi wengine kumuombea Dua Marehemu.

Kisomo hicho cha Hitma kimesomwa Nyumbani kwake Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Mabnodi  Mtaa wa Rahaleo Unguja.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni