Jumatano, 31 Julai 2019

MHE.AMINA IDDI: AING'ARISHA UWT ZNZ KWA NYENZO ZA KISASA,ASEMA MASLAHI YA CCM YAWEKWE MBELE.

 MWAKILISHI wa Viti Maalum Mkoa wa Magharib ambaye pia ni Mbunge kupitia Baraza la Wawakilishi  Mhe.Amina Idd Mabrouk(wa pili kushoto) akikabidhi Komputa Moja kwa Naibu Katibu Mkuu wa UWT Zanzibar Ndugu Tunu Juma Kondo(wa pili kulia) komputa hiyo kwa ajili ya Matumizi ya Ofisi ya Naibu Katibu Mkuu huyo.

 NAIBU Katibu Mkuu wa UWT Zanzibar Ndugu Tunu Juma Kondo(wa pili kulia) akimkabidhi Komputa Moja Katibu wa UWT Mkoa wa Magharibi Ndugu Zuwena Suleiman Mohamed (wa kwanza kushoto) kwa ajili ya Matumizi ya Ofisi ya Mkoa huo,iliyotolewa na  Mwakilishi wa Viti Maalum Mkoa wa Magharib ambaye pia ni Mbunge kupitia Baraza la Wawakilishi Mhe.Amina Idd Mabrouk(wa pili kushoto).

  NAIBU Katibu Mkuu wa UWT Zanzibar Ndugu Tunu Juma Kondo(wa pili kulia) akimkabidhi Komputa Moja Katibu wa UWT  Wilaya ya Mfenesini (wa kwanza kushoto Pili Issa Juma) kwa ajili ya Matumizi ya Ofisi ya Wilaya hiyo,iliyotolewa na  Mwakilishi wa Viti Maalum Mkoa wa Magharib ambaye pia ni Mbunge kupitia Baraza la Wawakilishi Mhe.Amina Idd Mabrouk (wa pili kushoto).

 NAIBU Katibu Mkuu wa UWT Zanzibar Ndugu Tunu Juma Kondo(kulia),akimkabidhi Komputa Moja Katibu wa UWT Wilaya ya Dimani Ndugu Sunna Said Mzee(wa kwanza kushoto),Komputa hiyo imetolewa na Mwakilishi wa Viti Maalum Mkoa wa Magharib ambaye pia ni Mbunge kupitia Baraza la Wawakilishi Mhe.Amina Idd Mabrouk(wa pili kushoto).

 MWAKILISHI wa Viti Maalum Mkoa wa Magharib ambaye pia ni Mbunge kupitia Baraza la Wawakilishi Mhe.Amina Idd Mabrouk, akizungumza katika Hafla hiyo ya utoaji wa Komputa hizo, katika Hafla iliyofanyika Ofisi za CCM Kiembe Samaki Unguja.

 NAIBU Katibu Mkuu wa UWT Zanzibar Ndugu Tunu Juma Kondo akizungumza katika Hafla ya utoaji wa komputa hiyo iliyofanyika katika Ofisi za CCM Kiembe Samaki Unguja.
 MWENYEKITI wa UWT Mkoa wa Magharibi Unguja akizungumza katika Hafla ya utoaji wa Komputa zilizotolewa na Mwakilishi wa Viti Maalum Mkoa wa Magharib ambaye pia ni Mbunge kupitia Baraza la Wawakilishi Mhe.Amina Idd iliyofanyika katika Ofisi za Chama Cha Mapinduzi Kiembe samaki Znz.

 VIONGOZI na Wanachama wa UWT wa Mkoa wa Magharibi wakiwa katika hafla ya kukabidhi komputa nne ya Mwakilishi wa Viti Maalum Mkoa wa Magharib ambaye pia ni Mbunge kupitia Baraza la Wawakilishi Mhe.Amina Idd Mabrouk, iliyofanyika katika Ofisi za CCM Kiembe Samaki Unguja.


MWAKILISHI wa Viti Maalum Mkoa wa Magharibi ambaye pia ni Mbunge kupitia Baraza la Wawakilishi Mhe.Amina Idd Mabrouk,amewasihi Viongozi na Wanachama wa CCM kufanya Kazi za Chama Cha Mapinduzi kwa bidii ili kuandaa Mazingira rafiki ya Ushindi wa Mwaka 2020.  

Rai hiyo aliitoa wakati akikabidhi Komputa Nne zenye Thamani ya Shilingi Milioni Nane kwa Ofisi za UWT Zanzibar ambazo ni Afisi Kuu ya UWT Zanzibar, UWT Mkoa wa Magharib,UWT Wilaya ya Dimani na UWT Wilaya ya Mfenesini ambapo kila Ofisi imekabidhiwa komputa Moja,Hafla hiyo imefanyika katika Ofisi za CCM huko Kiembembe Samaki Unguja.

Mhe.Amina amesema ili Chama kishinde katika Uchaguzi Mkuu ujao kila mwanachama anatakiwa kuweka mbele maslahi ya CCM badala ya maslahi binafsi.

Katika maelezo yake Mhe.Amina, ameeleza kuwa Vifaa hivyo ni mwendelezo wa Utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2015/2020,ikiwa ni sehemu ya kutekeleza kwa vitendo ahadi alizozitoa kwa Wananchi.

Pamoja na hayo amewaahidi Akina Mama wa Mkoa wa Magharibi kuwa ataanzisha Vikundi vya Ujasiriamali ili kuwakwamua kiuchumi na waweze kujiajiri wenyewe na kuondokana katika wimbi la umaskini. 

Amewasihi  Viongozi na Wanachama wa UWT kuthamini juhudi za kimaendeleo zinazofanywa na Viongozi hao ili wazidi kupata nguvu na Uthubutu wa kutatua changamoto zinazowakabili Wananchi.

Akizungumza katika Hafla hiyo Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu wa UWT Zanzibar Ndugu Tunu Juma Kondo,amempongeza  Mbunge huyo Mhe. Amina na Viongozi mbali mbali wa Mkoa huo ambao wamekuwa karibu na Wananchi kwa kutekeleza kwa Vitendo Ilani ya CCM.

 Ndugu Tunu, amewataka Viongozi na Watendaji waliokabidhiwa Komputa hizo kuzitunza vizuri ili zitumike kwa malengo yaliyokusudiwa katika kuhakikisha shughuli za kiutendaji za UWT zinatekelezwa kwa ufanisi zaidi.

Amesema Viongozi wa Chama na Serikali wanatakiwa kufuata nyayo za Viongozi Wakuu ambao ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein pamoja na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli kwa katika kuwatumikia Wananchi kwa uadilifu.

Awali Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Magharibi Ndugu Zainab Ali Maulid,amesema Umoja na Mshikamano ndio siri ya mafanikio ya kuimarika kwa Umoja huo.
  


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni