Jumapili, 14 Julai 2019

MHE.FAHARIA AKABIDHI VIFAA VYA TSH.MILIONI 15 KWA UWT MAJIMBO 9 YA MKOA WA MJINI.



MWENYEKITI wa UWT Mkoa wa Mjini Unguja Bi.Ghanima Sheha akifungua Kikao cha Baraza Kuu la Mkoa huo,huko katika Ukumbi wa Mkoa wa Mjini ulioopo Amani Unguja.

MBUNGE wa Viti Maalum wa Mkoa wa Mjini Mhe.Faharia Khamis  Shomari akizungumza na Wajumbe wa Baraza Kuu la UWT Mkoa wa Mjini kabla ya kukabidhi Vifaa.


BAADHI ya Wajumbe wa Baraza Kuu la UWT  Mkoa wa Mjini wakisikiliza nasaha za mgeni rasmi katika Ufunguzi wa Kikao cha Baraza Kuu la UWT Mkoa wa Mjini, kilichofanyika katika Ukumbi wa CCM Mkoa wa Mjini Unguja.


MBUNGE wa Viti Maalum wa Mkoa wa Mjini Mhe.Faharia Khamis Shomari (kulia),akimkabidhi Viti 50 Katibu wa UWT Jimbo la Magomeni Ndugu Khadija Rajab Pazi (kushoto).

MBUNGE wa Viti Maalum wa Mkoa wa Mjini Mhe.Faharia Khamis  Shomari(kulia) akimkabidhi Viti 50 Katibu wa UWT Jimbo la Kikwajuni Ndugu Amina Hassan Suleiman.


MBUNGE wa Viti Maalum wa Mkoa wa Mjini Mhe.Faharia Khamis  Shomari(kulia) akimkabidhi Viti 50 Katibu wa UWT Jimbo la Malindi Ndugu Salma Said Muumin.

MBUNGE wa Viti Maalum wa Mkoa wa Mjini Mhe.Faharia Khamis  Shomari akimkabidhi Katibu wa UWT Wilaya ya Amani Ndugu Asha Mzee Kiti Kimoja na Meza Moja vya Ofisi.

 MWAKILISHI wa Viti Maalum Mkoa wa Mjini ambaye pia ni Naibu Spika wa Baraza la Wawakiklishi Zanzibar Mhe.Mgeni Hassan Juma,akizungumza katika hafla hiyo ya kukabidhi Vifaa kwa Akina Mama wa UWT wa Majimbo 9 ya Mkoa wa Mjini.

 KATIBU wa UWT Mkoa wa Mjini Ndugu Stamili akitoa ufafanuzi wa masuala mbali mbali ya Kiutendaji katika Kikao cha Baraza Kuu la UWT  Mkoa huo kilichofanyika sambamba na kukabidhi Vifaa kwa Akina Mama.

 MWAKILISHI wa Viti Maalum Mkoa wa Mjini Mhe.Saada Ramadhan,akizungumza katika hafla hiyo.



MBUNGE wa Viti Maalum wa Mkoa wa Mjini Mhe.Faharia Khamis Shomari,amekabidhi Vifaa mbali mbali vyenye Thamani ya Shilingi Milioni 15 kwa Majimbo yote ya UWT ndani ya Mkoa huo.

Vifaa vilivyotolewa ni pamoja na Viti 451,Meza Moja ya Ofisi na  Mashine  Moja ya kutengenezea Chaki ikiwa ni sehemu ya kuunga Mkoa juhudi za Ujasiliamali za Akina Mama wa Mkoa huo.

Akizungumza katika hafla ya kukabidhi Vifaa hivyo Mbunge huyo Mhe.Faharia amesema lengo la kutoa Vifaa hivyo ni kutekeleza Ilani ya CCM ya Mwaka 2015/2020.

Mhe.Faharia ameeleza kuwa Akina Mama wa UWT ndani ya Mkoa huo pamoja na majukumu ya kisiasa waliyokuwa nayo bado wanatakiwa kujiajiri wenyewe kupitia ujasiriamali hivyo vifaa vilivyotolewa vitawasaidia katika harakati hizo za kujiajiri wenyewe.

Pamoja na hayo alitoa Wito kwa Wanawake wa rika mbali mbali ndani ya Mkoa wa Mjini kushiriki kaiunga Mkoa CCM ili ishinde katika Uchaguzi Mkuu ujao wa mwaka 2020.

Katika hafla hiyo Wawakilishi wa Viti Maalum wa Mkoa huo ambao ni Mhe.Mgeni Hassan Juma ameahidi kutoa Mashine mbili za Photocopy kwa UWT Wilaya ya Amani na Mjini huku Mhe.Saada Ramadhan amekabidhi Mifuko Mitano ya Jipusamu kwa ajili ya kutengenezea chaki na kuahidi shilingi Milioni Moja kwa kila Wilaya zilizomo katika Mkoa huo.

Wakizungumza kwa wakati tofauti Makatibu wa UWT wa Majimbo yote yaliyomo katika Mkoa huo, wameahidi Vifaa hivyo kuvitunza na kuhakikisha wanavitumia katika matumizi yaliyokusudiwa.

Awali akifungua Kikao cha Baraza Kuu la UWT Mkoa wa Mjini Mwenyekiti wa Mkoa huo Ndugu Ghanima Sheha,amesema Kikao hicho kitajadili masuala mbali mbali ya kiutendaji na kutoa maelekezo ya kiutendaji juu ya ufanikishaji wa majukumu mbali mbali ya UWT na CCM kwa ujumla.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni