Jumatano, 15 Julai 2015

Mimi na Rais Kikwete tumebeba dhamana ya kulinda amani

Rais wa Zanzibar dk.Ali Mohamed Shein amewaonya wanasiasa na kusema hakuna mtu aliyepo juu ya sheria ambapo yeye na rais Jakaya Kikwete wamebeba dhima kubwa ya kuhakikisha nchi inakuwa na utulivu mkubwa wakati wowote.

Dk.Shein alisema hayo muda mfupi baada ya kurejesha fomu ya kuomba ridhaa ya chama cha mapinduzi kuchaguliwa kuongoza Zanzibar kwa kipindi chengine cha miaka mitano hapo Afisi kuu ya CCM Kisiwandui mjini hapa.

Dk.Shein ambaye ni makamo mwenyekiti wa chama cha mapinduzi Zanzibar alitumia nafasi hiyo kuwashukuru wanachama wa chama hicho ambao walichukuwa jukumu la kumdhamini kwa ajili ya kuwania nafasi hiyo.

Alisema wapo wanasiasa wengine wanatumia nafasi ya kuwepo kwa serikali ya umoja wa kitaifa kwa ajili ya kuvuruga amani na utulivu jambo ambalo haliwezi kukubalika hata kidogo.

‘Mimi na rais Jakaya Kikwete ndiyo tuliyokabidhiwa jukumu la kuhakikisha Tanzania inakuwa taifa salama lenye amani na utulivu kwa muda wote’alisema dk.Shein huku akiahidi uchaguzi mkuu utakuwa huru na haki.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni