Jumamosi, 14 Machi 2015

Watakiwa kuhakikisha katiba pendekezi inapigiwa kura ya Ndio

Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Ndugu Vuai ali Vuai amewataka viongozi na watendaji wa CCM wa Mikoa na Wilaya kuhakikisha kuwa Katiba inayopendekezwa inapigiwa kura ya ndio na inapita hapo wakati wa kuuipigia kura ya maoni.

Naibu Katibu Mkuu huyo aliyasema hayo leo huko Kendwa katika hoteli ya Palumbo wakati alipokuwa anafungua mafunzo Elekezi kwa Watendaji na Viongozi wa Chama Cha Mapinduzi wa Mikoa na Wilaya za Zanzibar.

Ndugu Vuai aliwaeleza washiriki wa Mafunzo hayo Elekezi kuwa Chama chetu hivi sasa kimekabiliwa na mambo makuu matatu likiwemo la kura ya maoni ya kupitisha katiba inayopendekezwa na Uchaguzi Mkuu wa wa 2015 na tuhakikishe kuwa Chama cha Mapinduzi kinashinda kwa kishindo ili kiendelee kuongoza Dola ya Tanzania.
Kidumu Chama cha Mapinduzi!

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni