Jumatatu, 23 Machi 2015

Mh. Vuai akonganyoyo za wananchi wa kusini Unguja



Chama Cha Mapinduzi (CCM) ndio Chama pekee nchini chenye uwezo wa kudumisha amanina utulivu wa kitaifa, hivyo wananchi wana kila sababu ya kukichagua katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu, ili kiendelee kuongoza dola.
Kauli hiyo imetolewa na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Ndugu Vuai Ali Vuai, alipokuwa akiwa hutubia wananchi wa Wilaya ya Kusini Unguja kupitia mkutano wa hadhara uliofanyika katika kiwanja cha mpira cha Paje.

Amesema CCM ndio Chama pekee chenye sera, dira na dhamira ya kweli ya kuwakomboa wanyonge wa taifa hili nakuwaletea maendeleo endelevu ndani ya maeneo yao, hivyo wananchi wana kila sababu ya kukichagua na kukirejesha tena madarakani katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu.
Amesema kutokana na Utekelezaji kwa asilimia kubwa wa Ilani ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 - 2015 sambamba na ahadi mbali mbali zilizowekwa na Viongozi wa Chama hicho, wakati wa kampeni kuliko fanywa na  Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, nidhahiri wananchi watakiunga mkono CCM.

Akizungumzia kuhusu Katiba Pendekezwa, Naibu Katibu Mkuu huyo wa CCM (Z) amewataka wana CCM kushikamana na kutumia muda ulisalia kabla ya kura ya maoni, kutoa elimu kwa wananchi juu ya ubora wa Katiba hiyo, ili waweze kuielewa na kuipigia kura wakati utakapowadia.
Amesema elimu hiyo itawasaidia kwa kiasi kikubwa wananchi walio wengi kuwajengea uelewa mpana na hivyo kuipigia kura ya ndio Katiba hiyo, hapo Aprili 30, mwaka huu.

Amesema Katiba hiyo imezingatia maslahi ya makundi yote ya kijamii ya pande zote mbili za Muungano, kinyume na inavyopotoshwa na wanasiasa wa vyama vya upinzani kwa kuweka mbele matakwa ya vyama vyao Zaidi kuliko wananchi.

Ametoa wito kwa Wana CCM hasa waliokuwa Wajumbe wa Bunge la Katiba kutumia vikao vya Chama na mikutano ya hadhara kufafanua kwa kina vipengele mbali mbali vya katiba hiyo, mbele ya Wana CCM na Wazanzibari wote fursa zilizomo ndani ya katiba hiyo, kwani ndio mkombozi wao.

“Katiba hii Inayopendekezwa ndio mkombozi kwa Watanzania hasa Wazanzibari kwa vile  inatoa fursa kubwa kwa uchumi na ustawi wa Zanzibar na wananchi wake, hali inayopunguza kwa kiasi kikubwa yalemanung’uniko yaliyokuwepo ndani ya Katiba ya mwaka 1977.
Amesema wapinzani wamekuwa mstari wa mbele kuibeza Katiba hiyo, kutokana na ukweli kwamba walifahamu fika kuwa walikwisha shindwa hata kabla ya kuwasilishwa kwenye Bunge Maalum la Katiba.

“Wanachokifanya viongozi wa ukawa ni kufitinisha wananchi watekeleze matakwa yao, ili waikatae, lakini CCM tunawaambia ya guju kamwe hawawezi kutimiza ndoto yao hiyo”.AlisisitizaVuai.

Alitumia nafasi hiyo kumpasha Mansour Yussuf Himid, kutokana na madai yake ya kuwaonea uchugngu Wazanzibari, kwa kusema haina chembe ya ukweli na iwapo angekuwa na uchungu wa kweli asingewanyang’anya wazalendo mapande makubwa ya ardhi, majumba ya kuishi, mashamba, nk. Hivyo awarejeshee wenyewe.

Mapema,Naibu katibu Mkuu wa CCM Zanzibar  Vuai Ali Vuai,aliwakabidhi kadi za CCM jumla ya wanachama wapya 113 waliojiunga na chama hicho, ikiwa ni juhudi ya viongozi wa CCM wa wilaya hiyo ya awamu ya tatu ya mradi wa kuimarisha chama hicho.

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI.



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni